Friday, March 24, 2017

BECKENBAUER AWEKWA MTU KATI USWISI.

NGULI wa soka wa Ujerumani, Franz Beckenbauer amehojiwa na waendesha mashitaka nchini Uswisi juu ya tuhuma za ufisadi katika Kombe la Dunia mwaka 2006. Beckenbauer amekuwa akichunguzwa sambamba na wajumbe watatu wengine waliokuwepo katika kamati ya maandalizi ya michuano hiyo. Wanne hao wanatuhumiwa kwa udanganyifu, usimamizi mbaya wa kijinai, kutakatisha fedha na ubadhilifu. Beckernbauer ambaye aliongoza kamati hiyo mwaka 2000 amekanusha tuhuma zozote za rushwa katika kinyanyiro hicho cha kutafuta uenyeji wa michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment