Friday, March 31, 2017

CONTE AMKOMALIA HAZARD.

MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte amesisitiza Eden Hazard anafurahi kuwepo Stamford Bridge lakini amekubali tetesi za kuhitajika na klabu zingine zinaweza kuwaweka katika wakati mgumu wachezaji. Tetesi za hivi karibuni zinamuhusisha Hazard kuwaniwa na Real Madrid kwa kitita cha paundi milioni 100 majira ya kiangazi, ingawa nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji amesisitiza kuwa yeye na familia wanafurahia maisha ya London. Conte amesema hafahamu kama maofisa wa Chelsea watakubali ofa rasmi ya usajili kwa Hazard lakini anadhani mazungumzo yanayoendelea pembani kuhusiana kuhusiana na mkataba wake yanaweza kufanya akili ya mchezaji isitulie. Conte aliendelea kudai kuwa anachofahamu hivi sasa ni kuwa Hazard bado ni mali ya Chelsea na anafurahia kuwepo hapo.

No comments:

Post a Comment