Wednesday, March 15, 2017

FIFA YAMPIGA KITANZI CHABUR.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limemuengua rais wa zamani wa Shirikisho la Soka la Sudan Kusini Chabur Alei kugombea nafasi ya ujumbe katika baraza la shirikisho katika uchaguzi utakaofanyika Machi 16 mwaka huu jijini Addis Ababa. Akuzungumza na wanahabari, Chabur amesema Shirikisho la Soka la Afrika-CAF lilimuarifu kuhusu uamuzi huo wa FIFA ingawa hajapokea nyaraka yeyote ya maandishi. Hata hivyo, Chabur aliendelea kudai kuwa amekubaliana na maamuzi hayo na kama binadamu anafahamu utakuwepo wakati mwingine atakaopata nafasi nyingine. Chini ya sheria mpya za FIFA, mtu yeyote ambaye anashikilia au anataka kushikilia nafasi katika shirikisho hilo anatakiwa kufaulu uchunguzi wa kimaadili kabla ya uchaguzi.

No comments:

Post a Comment