Wednesday, March 15, 2017

UWANJA ALIOULALAMIKIA MOURINHO WAFUNGIWA.

WIKI moja baada ya Jose Mourinho kuponda sehemu ya kuchezea, Ligi Kuu ya Urusi imeufungia uwanja wa FC Rostov kutumika katika mechi zake za ligi kufuatia nyasi zake kuharibika. Manchester United ilitoka sare ya bao 1-1 katika Uwanja wa Olimp-2 katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa Europa League hatua ya 16 bora Alhamisi iliyopita. Akizungumza na wanahabari kabla ya mchezo huo, Mourinho alidai ni vigumu kwake kuamini atakwenda kuwa wanakwenda kucheza katika uwanja kama ule. Rostov sasa wamepewa mpaka Machi 24 kuuboresha uwanja wao huo kabla ya kuruhusiwa kuutumia tena kwa ajili ya mechi zao za ligi. United itavaana na United katika mchezo wa mkondo wa pili wa Europa League utakaofanyika Uwanja wa Old Trafford.

No comments:

Post a Comment