Friday, March 31, 2017

KLOPP AMLILIA LALLANA.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp hamlaumu kocha wa timu ya taifa ya Uingereza Gareth Southgate kwa kuumia kwa Adam Lallana lakini hajafurahishwa kwa mshambuliaji huyo kuchezeshwa mechi mbili za kimataifa. Lallana mwenye umri wa miaka 28, aliumia msulu wakati wa mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Lithuania Jumapili iliyopita baada ya kucheza ya kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Ujerumani Machi 22. Nyota huyo anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa muda wa mwezi mzima akianza kwa kukosa mchezo wa derby ya Merseyside kesho. Akizungumza na wanahabari, Klopp amesema hakufurahishwa na Lallana kuchezeshwa mchezo wa Jumatano iliyopita lakini sio kwamb anamlaumu Southgate. Klopp aliendelea kudai kuwa ingekuwa vyema kama waifanya kazi pamoja na kuulizana hili na lile wa manufaa ya pande zote mbili.

No comments:

Post a Comment