Friday, March 31, 2017

WENGER AWEZA WAZI MIKAKATI YAKE.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesisitiza wataendelea na kanuni yao la kushambulia pamoja na kukosolewa kuwa ndio imechangia kupoteza mechi zao nyingi. Arsenal wamepoteza mechi sita kati ya tisa zilizopita kwenye mashindano yote huku wakiporomoka mpaka nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu. Hatua hiyo imepelekea meneja huyo kuwa katika shinikizo kubwa huku mashabiki wakimtaka kuachia ngazi. Akizungumza na luninga ya Sky Sports, Wenger amesema kwasasa wamebakisha mechi 11 hivyo itakuwa sio busara kubadili kabisa aina yao ya uchezaji. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa wachezaji hao hao ndio walioshinda mechi na hao hao pia ndio waliopoteza hivyo anadhani kwasasa wataendelea na aina yao ileile ya kushambuliaji.

No comments:

Post a Comment