Tuesday, March 28, 2017

LIVERPOOL KUWAKODIA NDEGE COUTINHO NA FIRMINO.


KLABU ya Liverpool inadaiwa kwa mara nyingine itakodi ndege ili kuwarejesha nyota wake Philippe Coutinho na Roberto Firmino kutoka katika majukumu ya kimataifa. Nyota hao wa kimataifa wa Brazil wanatarajiwa kucheza mechi ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia dhidi ya Paraguay jijini Sao Paulo Alfajiri ya kuamkia kesho hivyo kufanya kuwa na siku mbili pekee za kujiandaa kwa ajili ya mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Everton Jumamosi hii. Kama kila kitu kikienda kama kilivyopangwa, Coutinho na Firmino wanatarajiwa kurejea Liverpool kesho kabla ya kuripoti mazoezi Alhamisi hii. Liverpool imeshakodi ndege mara kadhaa msimu huu ili kuhakikisha baadhi ya nyota wake wanaripoti klabuni kwa wakati. Mapema mwezi mwaka huu Sadio Mane alitumiwa ndege ya kukodi kutoka katika michuano ya Mataifa ya Afrika muda mfupi baada ya Senegal kuenguliwa katika michuano hiyo. Novemba mwaka jana taarifa zinadai kuwa Liverpool iligawana gharama za ndege ya kukodi na Manchester City, Chelsea na Paris Saint-Germain ili waweze kuwarejesha nyota wao wa

No comments:

Post a Comment