Tuesday, March 14, 2017

MOURINHO AWAJIBU MASHABIKI WA CHELSEA BAADA YA KUMZOMEA.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amewaambia mashabiki wa Chelsea kuwa bado yeye ni namba moja baada ya kuzomewa wakati wa mchezo wao wa Kombe la FA katika Uwanja wa Stamford Bridge. Mourinho aliyetimuliwa mara mbili Chelsea, aliitwa Yuda wakimaanisha msaliti na mashabiki wakati United ilipotandikwa bao 1-0, na yeye kujibu kwa kuonyesha vidole vitatu akimaanisha mataji matatu aliyoshinda. Mourinho amesema mpaka wana meneja mmoja aliyewasaidia kushinda mataji manne ya Ligi Kuu hivyo bado yeye namba moja. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa mpaka hapo itakavyobadilika vinginevyo, Yuda ataendelea kuwa namba moja.

No comments:

Post a Comment