Friday, March 24, 2017

POLISI WAKAMATA COCAINE ILIYOKUWA IMEWEKEWA PICHA YA MESSI.

POLISI nchini Peru wamekamata kilo 1,417 za cocaine jana, nyingi kati ya hizo zikiwa zimefungwa na kuwekwa picha ya mshabuliaji nyota wa kimataifa wa Argentina na klabu ya Barcelona Lionel Messi. Mzigo huyo wa madawa ya kulevywa unaokadiriwa kuwa thamani ya dola milioni 85, ulikamatwa ukiwa umefungwa kwenye vishurushi ambavyo juu yake waliweka picha ya Messi akiwa na jezi ya Barcelona. Polisi nchini humo wamedai kuwa madawa hayo yalikuwa yakisafirishwa kupelekwa nchini Ubelgiji. Hii ni mara ya pili kwa shehena kubwa ya madawa ya kulevya kukamatwa nchini Peru ya kwanza ikiwa ni Januari wakati polisi walipokamata madawa yenye zaidi ya thamani ya dola milioni 174.

No comments:

Post a Comment