Friday, March 10, 2017

RAKITIC AONGEZWA MKATABA BARCELONA.

KIUNGO wa Barcelona Ivan Rakitic ameongeza mkataba mwingine wa kuitumikia klabu hiyo ambao utamalizika mwaka 2021. Rakitic mwenye umri wa miaka 28, alianza katika mchezo wa juzi ambao Barcelona walitoka nyuma wakiwa wamefungwa mabao 4-0 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kabla ya kupindua matokeo na kushinda mabao 6-1 dhidi ya Paris saint-Germain. Taarifa za kuongezwa mkataba Rakitic zilithibitishwa katika tovuti ya Barcelona huku mkataba wake ukiwa umewekwa kitenzi cha euro milioni 125 kwa klabu itakayomuhitaji kabla ya mkatab wake kumalizika. Rakitic ameshinda mataji nane toka ajiunge na Barcelona akitokea Sevilla mwaka 2014.


No comments:

Post a Comment