Monday, March 27, 2017

WENGER HAWEZI KUNIFANYIA HIVI - OZIL.

KIUNGO wa Arsenal, Mesut Ozil amesema haamini kama kuna ukweli wowote juu ya taarifa kuwa meneja Arsene Wenger anataka kumuuza. Gazeti la Daily Express liliripoti wiki iliyopita kuwa Ozil na Alexis sanchez wanaweza kuuzwa na Wenger kufuatia nyota hao kuwa bado hawajaongeza mikataba ambayo inatarajiwa kumalizika mwaka 2018. Akizungumza na wanahabari kuhusiana na suala hilo, Ozil amesema hadhani kama taarifa hizo zina ukweli wowote kwani Wenger asingeweza kusema taarifa hizo bila kumshirikisha. Nyota huyo wa zamani wa Real Madrid aliendelea kudai kuwa bado anafurahia kuwepo Arsenal lakini kwasasa kuna kitu hakiendi sawa kwa timu ndio maana wamekuwa hawapati matokeo mazuri. Hata hivyo, Ozil anaamini upepo huo mbaya utapita na watarejea katika makali yao hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment