Friday, March 17, 2017

YAYA TOURE ANOGEWA MAN CITY.

KIUNGO wa Manchester City, Yaya Toure amesema Pep Guardiola ni sababu kubwa ya yeye kufanikiwa kurejea katika kiwnago chake na anataka kuendelea kubaki Etihad baada ya msimu huu. Nyota huyo aliachwa katika mipango ya City mwanzoni mwa msimu baada ya kutokea msuguano baina yake na Guardiola hali ambayo ilitishia mustakabali wake. Hata hivyo, Toure aliejeshwa katika kikos cha kwanza baada ya kuomba radhi kwa meneja huyo na sasa anataka kuendelea kubakia klabuni hapo baada ya mkataba wake wa sasa kumalizika. Akizungumza na wanahabari, Toure amesema anaipenda City na bado anapenda kuendelea kuitumikia mpaka pale atakapohisi mwili wake umefikia ukingoni.

No comments:

Post a Comment