Monday, April 17, 2017

CONTE AKUBALI LAWAMA KIPIGO CHA MAN UNITED.

MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte amesema anakubali kulaumiwa kwa kushindwa kuwapa morari wachezaji wake kufuatia kipigo cha mabao 2-0 walichopata kutoka Manchester United jana. Kipigo hicho walichopata Old Trafford kinawafanya kutofautiana alama nne pekee dhidi ya Tottenham Hotspurs wanaoshikilia nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu. Conte amesema hawakucheza mchezo mzuri na United walistahili kushinda mchezo huo. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa United walionyesha nia na ari zaidi kwenye mchezo huo jambo ambalo wao hawakufanya hivyo ndio maana anakubali lawama.

No comments:

Post a Comment