Monday, April 17, 2017

MARC BARTA APATA UGENI WA WASHIKAJI.

BEKI mahiri wa Borussia Dortmund Marc Barta mwishoni mwa wiki hii amepata ugeni muhimu baada ya kutembelewa na wachezaji wenzake wa zamani wa Barcelona Jordi Alba na Sergio Busquets. Beki huyo wa kimataifa wa Hispania ndio pekee aliyeumia wakati basi la Dortmund liliposhambuliwa na mabomu wakati wkaiwa njiani kuelekea katika mchezo wao dhidi ya Monaco Jumanne iliyopita. Barta alifanyiwa upasuaji wa mkono na anatarajiwa kukosa mechi zote zilizosalia msimu huu kutokana na tukio hilo, lakini wakati akiwa kwenye wakati huo mgumu marafiki zake wawili wa karibu waliamua kumtembelea na kumjulia hali. Alba ambaye ametokea katika akademi ya Barcelona sambamba na Barta na Busquets, alituma picha ukurasa kwenye ukurasa wake wa Instagram wakiwa pamoja. Alba aliandika kwenye ukurasa wake huo kuwa anajisikia furaha kumuona rafiki yake na kucheka pamoja naye.

No comments:

Post a Comment