Friday, April 14, 2017

ZIDANE KUMPUMZISHA BALE.

WINGA wa Real Madrid, Gareth Bale anatarajiwa kukosa mchezo wa La Liga dhidi ya Sporting Gijon kesho kutokana na kutokuwa fiti. Kikosi cha Madrid kitakwenda kucheza mechi hiyo ya ugenini, mchezo ambao utafuatiwa na mechi mbili muhimu katika kipindi cha wiki moja. Mchezo wa mkondo wa pili war obo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich utafuatiwa siku tatu baadae, kabla ya Barcelona hawajakwenda Santiago Bernabeu kwa ajili ya El Clasico Jumapili ya Aprili 23. Bado alipata majeruhi madogo katika mchezo wa mkondo wa kwanza walioshinda mabao 2-1 Allianz Arena na meneja Zinedine Zidane ameamua kumpumzisha ili kupona kabisa kabla ya mechi hizo mbili kubwa zijazo.

No comments:

Post a Comment