Saturday, April 29, 2017

PIRES AMTAKA MBAPPE KWENDA ARSENAL.


NGULI wa zamani wa soka wa Arsenal, Robert Pires amedai kuwa chipukizi wa Monaco Kylian Mbappe ataweza kunufaika kwa kiasi kikubwa kama akijiunga na klabu hiyo na kuongeza anadhani nyota huyo atakwenda huko. Hata hivyo, Pires amesema bado ni mapema sana kumfananisha nyota huyo na mshambuliaji nyota wa zamani wa timu hiyo Thierry Henry. Mbappe mwenye umri wa miaka 18 anatajwa kama mmoja kati ya wachezaji bora kabisa wanaochipukia duniani kufuatia kiwango bora alichoonyesha kwa klabu ya Monaco iliyotinga nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Pires ambaye aliwahi kucheza na henry katika kikosi cha Arsene Wenger miaka ya 2000 anaamini Arsenal ndio sehemu sahihi kwa Mbappe kukua na kuimarika kama mchezaji.

No comments:

Post a Comment