Wednesday, May 24, 2017

ARSENAL KUMKOSA GABRIEL KOMBE LA FA.

BEKI wa Arsenal, Gabriel anatarajiwa kukosa mchezo wa Jumamosi hii wa Kombe la FA dhidi ya Chelsea utakaofanyika katika Uwanja wa Wembley kufuatia madaktari kuthibitisha kuwa anaweza kuwa fiti baada ya wiki nane au zaidi. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 alibebwa katika machela katika mchezo wa Jumapili hii dhidi ya Everton baada ya kuumia goti. Beki mwenzake Laurent Koscielny pia anatarajiwa kukosa mchezo huo baada ya Chama cha Soka cha Uingereza kutupilia mbali rufani yake kupinga kadi nyekundu aliyopewa kwenye mchezo dhidi ya Everton. Beki mwingine anayecheza nafasi ya kati Shkodran Mustafi naye yuko katika hatihati kufuatia kupata mtikisiko wa ubongo kufuatia kugongwa kichwani katika mchezo dhidi ya Sunderland wiki iliyopita.

No comments:

Post a Comment