Wednesday, May 24, 2017

YAYA TOURE ATOA MSAADA KWA WAHANGA WA MANCHESTER.

KIUNGO wa Manchester City, Yaya Toure na wakala wake kila mmoja anatarajiwa kutoa kitita cha paundi 50,000 sawa na zaidi ya milioni 145 za kitanzania, kwa ajili ya wahanga wa shambulio la bomu la kujitoa muhanga jijini Manchester. Mlipuko huo uliotokea katika Ukumbi wa Manchester Arena juzi uliacha watu 22 wakipoteza maisha huku wengine zaidi ya 59 wakijeruhiwa wakati wakihudhuria tamasha la Ariana Grande. Akizungumza na wanahabari wakala wa Toure, Dimitri Seluk amesema taarifa za binti wa miaka nane aliyekwenda kumtizama mwanamuziki aliyempenda halafu hakurudi nyumbani ni jambo la kuhuzunisha kwa kiasi kikubwa. Seluk aliongeza kuwa Toure na yeye wanataka kusaidia na njia pekee wanayoona inafaa kwasasa ni kutoa kiasi hicho cha fedha kusaidia wahanga na haijalishi kama wote wanatoka Manchester au la.

No comments:

Post a Comment