Wednesday, May 24, 2017

CAVALIERS WAPIGA HATUA MOJA KUELEKEA FAINALI YA NBA.

TIMU ya mpira wa kikapu ya Cleveland Cavaliers imebakisha ushindi katika mechi moja ili waweze kutinga katika fainali za NBA kwa mara ya tatu mfululizo baada ya kuichapa Boston Celtics kwa vikapu 112-99. Cavaliers sasa wanaongoza kwa 3-1 kati ya mechi saba za fainali ya Kanda ya Mashariki. Golden State Warriors tayari wameshatinga kwenye fainali hizo kwa kushinda mechi 4-0 dhidi ya San Antonio Spurs kwenye fainali ya Kanda ya Magharibi. Warriors walitawadhwa mabingwa wa NBA mwaka 2015 lakini walitandikwa mwaka jana na Cavaliers waliokata kiu yao ya kulikosa taji hilo kwa miaka 52. Nyota wa Cavaliers Kyrie Irving na LeBron James kwa pamoja walifunga alama 76 nyumbani kwa Celitcs, ambao walikuwa bila nyota wao Issaiah Thomas aliyekuwa majeruhi. Mchezo wa tano unatarajiwa kufanyika jijini Boston kesho.

No comments:

Post a Comment