Tuesday, May 23, 2017

MANJI ATUNDIKA DARUGA YANGA.

MWENYEKITI wa Klabu ya Yanga, Yussuf Manji, amejiuzulu wadhifa huo akidai kuwa anatoa nafasi kwa watu wengine kuiongoza.  Kupitia barua yake iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii, MANJI, amesema anaondoka akiamini ameiacha Yanga ikiwa timu yenye mafanikio makubwa ya kisoka hapa nchini. Licha ya taarifa yake hiyo, pia akizungumza kwenye kwenye mahojiano na Kituo Kimoja cha Radio jijini Dar es salaam, MANJI amekiri kujiuzulu wadhifa huo. Kwa mujibu wa barua ya MANJI iliyoisaini Mei 22, mwaka huu, amejiuzulu Uenyekiti na sasa majukumu yote hadi pale uchaguzi mpya utakapofanyika wa kujaza nafasi yake majukumu yote ya Timu yatakuwa chini ya Makamu wa Rais, Sanga. SANGA amethibisha kupokea barua ya MANJI kujiuzulu akisema ni kweli amepokea barua hiyo ya mwenyekiti juu ya uamuzi wake wa kupumzika kwa sasa.


No comments:

Post a Comment