Tuesday, May 23, 2017

HAKUNA TISHIO FAINALI YA EUROPA LEAGUE - UEFA.

SHIRIKISHO la Soka la Ulaya-UEFA limedai kuwa hakuna taarifa zozote za kiintelejensia zinazoonyesha kuwa fainali ya Europa League inaweza kuwa mlengwa wa shambulio kufuatia tukio lililotokea jijini Manchester. Watu wapatao 22 waliuawa na wengine 59 kujeruhiwa, wakiwemo watoto katika mlipuko uliotokea mwishoni mwa tamasha kwenye Ukumbi wa Manchester Arena jana. Polisi nchini Uingereza wamekuwa wakilichukua tukio kama la kigaidi huku Waziri Mkuu wake Theresa May akilaani vikali wote waliohusika. Tukio hilo limetokea ikiwa zimebaki saa chache kabla ya mchezo wa fainali ya Europa League kati ya Manchester United dhidi ya Ajax Amsterdam utakaofanyika jijini Stockholm, Sweden kesho. Kufuatia hofu hiyo, UEFA imewahakikishia mashabiki waliopanga kuhudhuria mchezo huo kuwa hali ya kiusalama ni shwari kabisa na hakuna tishio lolote lililoripotiwa mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment