Tuesday, May 23, 2017

GOLDEN STATE WARRIORS WATINGA FAINALI ZA NBA.

TIMU ya mpira wa kikapu ya Golden State Warriors imefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya NBA kwa mara ya tatu mfululizo kufuatia ushindi wa vikapu 129-115 dhidi ya San Antonio Spurs. Nyota wa Warriors Stephen Curry alifunga alama 36 na Kevin Durant alama 29 ambazo ziliisaidia kukamilisha ushindi wa 4-0 kati ya mechi saba za fainali ambazo zilipaswa kuchezwa katika Kanda ya Magharibi. Sasa Warriors wanasubiri bingwa mtetezi Cleveland Cavaliers au Boston Celtic ili waje kucheza naye fainali za NBA kuanzia Juni mosi mwaka huu. Cavaliers mpaka sasa wanaongoza kwa mechi 2-1 kwenye fainali ya Kanda ya Mashariki.

No comments:

Post a Comment