Tuesday, May 23, 2017

RAIS WA ZAMANI WA BARCELONA AKAMATWA.

RAIS wa zamani wa Barcelona, Sandro Rosell amekamatwa ikiwa ni sehemu ya uchunguzi kuhusiana na tuhuma za kutakatisha fedha. Watu kadhaa pia wamekamatwa na polisi kufuatia tuhuma hizo kaskazini mashariki mwa mji wa Barcelona. Polisi wamesema kukamatwa huko ni sehemu ya uchunguzi kuhusiana na haki za mauzo zinazohusiana na Brazil. Rosell alikuwa rais wa Barcelona kuanzia mwaka 2010 mpaka 2014, wakati alipojiuzulu kufuatia uamuzi wa mahakama ya Hispania kufanyia uchunguzi usajili wa nyota wa kimataifa wa Brazil Neymar mwaka 2013. Juni mwaka 2016, Barcelona ililipa faini ya euro milioni 5.5 juu ya uhamisho wa Neymar mwenye umri wa miaka 25 kutoka Santos. Mke wa Rosell ni miongoni mwa watu waliokamatwa katika sakata hilo la leo.

No comments:

Post a Comment