Tuesday, May 23, 2017

CONTE ATWAA TUZO YA KOCHA BORA WA LMA.

MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte ameshinda tuzo ya kocha bora wa msimu inayotolewa na Chama cha Makocha wa Ligi Kuu ya Uingereza-LMA. Meneja huyo raia wa Italia ametwaa tuzo hiyo kufuatia kuiongoza Chelsea kushinda taji la ligi katika msimu wake wa kwanza Stamford Bridge. Meneja wa klabu ya Brighton, Chris Hughton ameshinda tuzo ya kocha bora wa msimu wa Ligi ya Ubingwa kufuatia kuipandisha daraja timu hiyo. Meneja wa Sheffield United Chris Wilder na Paul Cook wa Portmouth nao wametwaa tuzo kufuatia kuziwezesha timu zao kupanda katika Ligi ya Ubingwa kutoka ligi daraja la kwanza. Conte ambaye timu yake imeweka rekodi ya kushinda mechi 30 za Ligi kuu, anaweza kutwaa taji la pili Jumamosi hii wakati watakapocheza na Arsenal katika fainali ya Kombe la FA.

No comments:

Post a Comment