Monday, May 22, 2017

SAFU YA ULINZI YA ARSENAL UTATA.

KLABU ya Arsenal inakabiliwa na tatizo kwenye safu yake ya ulinzi kuelekea mchezo wa fainali ya Kombe la FA dhidi ya Chelsea Jumamosi hii, kufuatia Shkodran Mustafi kuwa katika hatihati ya kutocheza kutokana na majeruhi. Beki huyo mwenye umri wa miaka 25 alijigonga kichwani katika mchezo dhidi ya Sunderland uliochezwa Jumanne iliyopita. Mustafi alimaliza kwenye mchjezo huo lakini alipata dalili za mtikisiko kwenye ubongo hatua ambayo ilipelekea kuachwa kwenye mchezo wa jana dhidi ya Everton. Beki mwingine Laurent Koscielny atakosa fainali hiyo itakayochezwa kwenye Uwanja wa Wembley akitumikia adhabu wakati Gabriel naye alitolewa nje kwa machela jana. Mustafi alijiunga na Arsenal kwa kitita cha paundi milioni 35 majira ya kiangazi na amefanikiwa kucheza mechi 37 katika klabu hiyo msimu huu.

No comments:

Post a Comment