Monday, May 22, 2017

JUVENTUS YAMUWANIA KEITA

MKURUGENZI mkuu wa Juventus, Giuseppe Marotta amethibitisha kuwa mabingwa hao wa Serie A wanamuwania mshambuliaji wa Lazio Balde Keita, lakini amedai hakuna makubaliano yeyote yaliyofikiwa. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23, amekuwa na msimu mzuri kufuatia kufunga mabao 16 katika mechi 31 za ligi alizoichezea Lazio. Kiwango chake hicho hakijaivutia Juventus pekee bali pia Manchester United na Chelsea lakini suala la usajili bado linaonekana kuwa mbali kwasasa. Akizungumza na wanahabari, Marotta amesema hakuna makubaliano yeyote yaliyoafikiwa juu ya Keita hivyo bado ni mchezaji wa Lazio na ana mkataba wa mwaka mmoja zaidi. Marotta aliendelea kudai kuwa wanamfuatilia Keita kwa karibu kwani wanataka kumsajili lakini kwasasa wametulia.

No comments:

Post a Comment