Monday, May 22, 2017

MMILIKI WA ARSENAL AKANUSHA KUTAKA KUUZA HISA ZAKE.

MWANAHISA mkubwa wa Arsenal, Stan Kroenke amesema hajwahi kutaka kuuza hisa zake anazomiliki kwenye klabu hiyo. Kampuni ya Kroenke inayojihusisha na masuala ya michezo na burudani ilitoa kauli hiyo mapema leo kufuatia taarifa kuwa Alisher Usmanov ametoa ofa ya paundi milioni moja kwa ajili ya kuchukua umiliki wa klabu hiyo. Katika taarifa yake kampuni hiyo ya Kroenke imeiongeza kuwa wamepanga kuwekeza Arsenal kwa kipindi kirefu na wanatarajia kubakia hivyo. Taarifa hiyo imekuja siku moja baada ya Arsenal kushindwa kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza baada ya kupita miaka 20. Kroenke anamiliki hisa asilimia 67 Arsenal, huku Usmanov yeye akimiliki hisa asilimia 30 lakini hashiriki vikao vya bodi au kutoa maamuzi ya klabu.

No comments:

Post a Comment