Monday, May 22, 2017

TOURE ATAKA KUSTAAFU AKIWA CITY.

KIUNGO wa Manchester City, Yaya Toure amesema anataka kumaliza soka lake akiwa na klabu hiyo na kuongeza kuwa itakuwa vigumu kuvaa jezi ya timu nyingine. Mkataba wa Toure unatarajiwa kumalizika Julai mwaka huu na sio yeye wala meneja Pep Guardiola aliyeweza kudokeza kama nyota huyo wa kimataifaw a Ivory Coast atapewa ofa ya mkataba mwingine. Beki Pablo Zabaleta aliagwa katika mchezo wa mwisho wa City kucheza nyumbani wiki iliyopita baada ya kuihabalisha klabu kuwa hataongeza mkataba mwingine pindi huu wa sasa utakapomalizika majira ya kiangazi. Akizungumza na wanahabari mara baada ya ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Watford jana, Toure amesema bado anahitaji kucheza zaidi kwani anaona bado ana uwezo wa kuisaidia City kupata mataji zaidi.

No comments:

Post a Comment