Friday, May 26, 2017

AUBAMEYANG MGUU NJE MGUU NDANI DORTMUND.

MSHAMBULIAJI wa Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang anataka kunyakuwa taji lake la kwanza akiwa na klabu hiyo kesho pamoja na tetesi kuwa mchezo huo wa fainali ya Kombe la Ujerumani unaweza kuwa wa mwisho kwenye timu hiyo. Dortmund wanatarajiwa kukwaana na Eintracht Frankfurt mchezo utakaofanyika katika Uwanja wa Olimpiki uliopo jijini Berlin. Dortmund wanataka kuondoa mkosi wa kufungwa katika fainali tatu zilizopita zilizochezwa jijini Berlin. Nahodha wa Dortmund, Marcel Schmelzer amesema kila wakati walipokuwa Berlin katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita wamekuwa wakirejea nyumbani wakiwa mikono mitupu. Nahodha huyo aliendelea kudai safari hii watajirekebisha kuhakikisha wanashinda mchezo huo na kuondoka na furaha. Naye Aubameyang amesema atazungumza na klabu hiyo na kufanya maamuzi baada ya fainali hiyo.

No comments:

Post a Comment