Friday, May 26, 2017

EVERTON KUJA DAR.

KLABU ya Everton inatarajiwa kuwa klabu ya kwanza inayoshiriki Ligi Kuu ya Uingereza kucheza Tanzania wakati watakapokuja kwa ajili ya mchezo wa kirafiki kujiandaa na msimu mpya. Mchezo huo unaoratibiwa na kampuni ya ya kamari ya SportPesa unatarajiwa kuchezwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Julai 13 mwaka huu. Klabu hiyo inatarajiwa kucheza na washindi wa SportPesa Super Cup, ambao unatarajiwa kushirikisha timu nne kutoka Kenya na nne kutoka Tanzania. Kampuni ya SportPesa yenye makao yake makuu nchini Kenya ndio wadhamini wapya wa jezi za Everton kuanzia msimu ujao.

No comments:

Post a Comment