Friday, May 26, 2017

ZABALETA KWENDA WEST HAM UNITED.

BEKI Pablo Zabaleta anatarajiwa kusaini mkataba na West Ham United akiwa kama mchezaji huru pindi mkataba wake na Manchester City utakapomalizika mwishoni mwa mwezi ujao. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 32, anatarajiwa kujiunga na West Ham kwa mkataba wa miaka miwili kuanzia Julai Mosi. Zabaleta anaondoka City baada ya kuitumikia kwa miaka tisa na kumfanya kuwa mchezaji wa tatu aliyeitumikia klabu hiyo kwa kipindi kirefu baada ya Joe Hart na Vincent Kompany. Akizungumza na wanahabri, Zabaleta amesema kubwa lililomfanya kuondoka City ni kutafuta changamoto mpya na anamatumaini ya kuisaidia West Ham katika malengo yake ya msimu ujao. Zabaleta ambaye amecheza mechi 22 za mashindano yote msimu huu akiwa na City, alijiunga nao akitokea Espanyol kwa kitita cha paundi milioni 6.5 mwaka 2008 na kufanikiwa kushinda mataji mawili ya Ligi Kuu, Kombe la FA na mataji mengine mawili ya Kombe la Ligi.

No comments:

Post a Comment