Friday, May 26, 2017

VALENCIA AONGEZA MKATABA UNITED.

WINGA wa Manchester United, Antonio Valencia amesaini nyongeza ya mwaka mmoja katika mkataba wake ambao utamuweka hapo mpaka mwaka 2019 huku kukiwa na kipengele cha kuongezewa tena. Valencia mwenye umri wa miaka 31 amecheza mechi 43 za mashindano yote za United msimu huu na kukiongoza kikosi cha timu hiyo kama nahodha wakati walipotwaa taji la Europa League mbele ya Ajax Amsterdam juzi. Nyota huyo wa kimataifa wa Ecuador alijiunga na United akitokea Wigan Athletic mwaka 2009. Akizungumza na wanahabari, Valencia amesema amefurahia sana mkataba huo kwani klabu hiyo imekuwa sehemu ya maisha yake toka alipojiunga nao mwaka 2009.

No comments:

Post a Comment