Thursday, May 18, 2017

BAYERN WASINGEPATA URAHISI UINGEREZA - KLOPP.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema Bayern Munich wasingeweza kupata urahisi wa Bundesliga kama ingekuwa klabu ya Ligi Kuu ya Uingereza. Klopp bado ndio meneja pekee aliyezima utawala wa Bayern kwenye soka la Ujerumani kufuatia kuingoza Borussia Dortmund kutwaa mataji mawili mfululizo ya Bundesliga mwaka 2011 na 2012. Toka kipindi hicho Bayern imerejea katika utawala wake huku Dortmund, Wolfsburg na RB Leipzig zikishindwa kuizuia timu hiyo. Bayern waliirarua Arsenal kwa jumla ya mabao 10-2 msimu huu katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Akihojiwa kuhusu nafasi ya Bayern kama ingekuwa klabu ya Uingereza, Klopp amesema haingekuwa rahisi kutwaa taji la ligi kama wanavyofanya kwenye Bundesliga.

No comments:

Post a Comment