Thursday, May 18, 2017

BENZEMA AACHWA TENA UFARANSA, DESCHAMPS ATOA SABABU.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ufaransa, Didier Deschamps amesema maelewano yaliyopo katika kikosi chake hawezi kuyahatarisha kwa kumuita tena mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema. Benzema hajaitwa katika kikosi cha Ufaransa toka aliposhitakiwa na polisi kwa tuhuma za kujihusisha na genge la watu waliokuwa wakimuandama mchezaji mwenzake wa nchi hiyo Mathieu Valbuena, kesi ambayo bado haijafikishwa mahakamani. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 mwaka jana alikosa michuano ya Ulaya iliyofanyika katika ardhi yao ya nyumbani kutokana na tuhuma hizo, ingawa rais wa Shirikisho la Soka la Ufaransa-FFF, Noel Le Grael tayari alishatangaza Februari kuwa uamuzi wa Benzema kuitwa unabaki kwa Deschamps. Hata hivyo, Benzema kwa mara nyingine amekosa kwenye kikosi hicho ambacho kinatarajiwa kucheza mechi tatu dhidi ya Paraguay, Sweden na Uingereza Juni mwaka huu.

No comments:

Post a Comment