Friday, May 19, 2017

MSIMU UJAO SITAFANYA MAKOSA - MOURINHO.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amesisitiza hatafanya makosa katika msimu wake wa pili Old Trafford haswa ikizingatiwa kuwa kwasasa anaifahamu vyema klabu hiyo kwa undani. Mourinho bado anaweza kumaliza msimu wake wa kwanza kwa kushinda mataji mawili kama akifanikiwa kuichapa Ajax Amsterdam katika fainali ya Europa League wiki ijayo baada ya kuwa tayari wameshatwaa taji la Kombe la Ligi. Lakini walishindwa kutamba katika Ligi Kuu na wanatarajiwa kumaliza katika nafasi ya sita katika msimamo pamoja na matokeo yeyote watakayopata katika mechi ya mwisho dhidi ya Crystal Palace Jumapili hii. Hiyo inamaanisha kuwa Europa League ndio nafasi yao ya pekee iliyobaki ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao. Akizungumza na wanahabari, Mourinho amesema msimu wa kwanza ulikuwa mgumu lakini anadhani atafurahia msimu wa pili kwakuwa anajua hataweza kufanya makosa.

No comments:

Post a Comment