Friday, May 19, 2017

POCHETTINHO AMMWAGIA SIFA KANE BAADA YA KUPIGA NNE.

MENEJA wa Tottenham Hotspurs, Mauricio Pochettino amesema Harry Kane ni mmoja kati ya washambuliaji bora duniani na kusisitiza kuwa klabu hiyo inaweza kuwabakisha wachezaji wake bora kwa ajili ya msimu ujao. Kane mwenye umri wa miaka 23, alifunga mabao manne katika ushindi wa mabao 6-1 waliopata Spurs dhidi ya Leicester City katika Uwanja wa King Power na kukwea mpaka kileleni kwenye orodha ya wafungaji bora akiwapita Romelu Lukaku na Alexis Sanchez. Akizungumza na wanahabari, Pochettino amesema Kane ni mchezaji muhimu na anayependa kuitumikia Spurs. Pochettino aliendelea kudai kuwa wachezaji wote wanaowahitaji watakuwepo kwa ajili ya msimu ujao na kama mchezaji yeyote ataondoka itakuwa ni juu ya klabu yenyewe. Kane aliyekuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu msimu uliopita kwa kufunga mabao 25, msimu huu tayari ameshafikisha mabao 26 huku kukiwa kumebaki mechi moja msimu kumalizika.

No comments:

Post a Comment