Friday, May 19, 2017

GRIEZMANN ATAJA ATAKAENYAKUA TUZO YA BALLON D'OR LAKINI SIO RONALDO.

MSHAMBULIAJI nyota wa Atletico Madrid, Antonio Griezmann hategemei kama mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo atashinda tuzo ya Ballon d’Or mwakani. Katika kipindi cha miaka 10 iliyopita tuzo hizo zimekuwa zikitawaliwa na nyota wawili Ronaldo na mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi huku Griezmann akiikaribia tuzo hiyo kwa kushika nafasi ya tatu mwaka jana. Lakini pamoja na wadau wengi kumpigia chapuo Ronaldo kutwaa tuzo hiyo baada ya kufunga mabao matano katika mechi za mikondo miwili dhidi ya Bayern Munich kabla ya kuja kufunga hat-trick dhidi ya Atletico na kutinga fainali, bado Griezmann haoni kama nyota huyo ataitwaa tuzo hiyo. Akizungumza na wanahabari, Griezmann amesema kwa mawazo anadhani Juventus ndio watakaotwaa taji la Ligi ya Mabingwa na Ulaya na kipa wao Gianluigi Buffon ndio atayetwaa tuzo hiyo badala ya Ronaldo.

No comments:

Post a Comment