Friday, May 19, 2017

WENGER KUFAHAMU MUSTAKABALI BAADA YA KOMBE LA FA.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema mustakabali wake katika klabu hiyo utaamuliwa katika kikao cha bodi baada ya fainali ya Kombe la FA Mei 27 mwaka huu. Meneja huyo raia wa Ufaransa, mwenye umri wa miaka 67 amekuwa na Arsenal toka mwaka 1996 na mkataba wake unamalizika kipindi hiki cha majira ya kiangazi. Wenger amekuwa akikabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo wengi wao wakimuhitaji aachie ngazi. Akizungumza na wanahabari, Wenger amesema kuna mambo yatajadiliwa katika mkutano huo wa bodi na moja kati yake ni juu ya kitakachotokea kwa meneja. Wenger aliendelea kudai kuwa yeye mwenyewe atakuwepo kwenye kikao hicho, lakini kwasasa wamehamishia nguvu zao katika mechi zao za mwisho. Arsenal watavaa na mabingwa wa Ligi Kuu Chelsea katika Uwanja wa Wembley.

No comments:

Post a Comment