Friday, May 19, 2017

KALOU AITWA TENA IVORY COAST.

KOCHA mpya wa Ivory Coast, Marc Wilmots ametaja kikosi chake kwanza toka alipoteuliwa kuchukua kibarua hicho machi mwaka huu. Ivory Coast inakabiliwa na mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Uholanzi Juni 4 na mchezo mwingine wa kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika siku tano baadae dhidi ya Guinea. Katika kikosi hicho cha wachezaji 27, Wilmots amemjumuisha winga wa Hertha berlin Salomon Kalou ambaye anaonekana bado ataendelea kucheza soka la kimataifa. Kalou alikuwa akifikiria mustabali wake ujao kwa soka la kimataifa baada ya Ivory Coast waliokuwa mabingwa watetezi walipoenguliwa katika michuano ya Mataifa ya Afrika mapema mwaka huu. Wilmots ambaye kabla ya kutua Ivory Coast alikuwa akiinoa Ubelgiji, pia amemjumuisha mshambuliaji aliyekosekana kwa kipindi kirefu Seydou Doumbia.

No comments:

Post a Comment