Thursday, May 18, 2017

VURUGU ZASABABISHA MCHEZO KUSITISHWA.

MECHI ya hatua ya mtoano kutafuta nafasi ya kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao kati ya Panathinaikos na PAOK Salonika imelazimika kusitishwa kufuatia kutoka kwa vurugu. Mchezo huo ulishuhudia mwamuzi akitoa kadi nne nyekundu, mashabiki wakipigana wenyewe kwa wenyewe huku kocha wa PAOK Vladimir Ivic akipigwa na chupa ya maji kichwani na kukimbizwa hospitali. Panathinaikos ilikuwa ikiongoza kwa bao 1-0 katika mchezo huo kabla ya mwamuzi kuamua kusitisha katika dakika ya 55. Kabla ya kusitisha mchezo huo kabisa mwamuzi Giorgos Kominos aliusimamisha kwa muda wakati kocha Ivic akipatiwa matibabu ya awali kabla ya kukimbizwa hospitali na kushonwa nyuzi kadhaa. PAOK, Panathinakos, AEK Athens na Panionios zote zipo kwenye hatua ya mtoano kutafuta mshindi mmoja ambaye ataungana na mabingwa wa Ligi Kuu ya Ubelgiji, Olympiakos katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.

No comments:

Post a Comment