Thursday, May 18, 2017

MOURINHO ALIA NA WASIMAMIZI WA LIGI KUU.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amesema inakatisha tama kuwa Ligi Kuu ya Uingereza haijali kuhusu kuzisaidia timu za Uingereza zikiwa na mechi katika michuano ya Ulaya. United inatarajiwa kupambana na Crystal Palace katika mchezo wao wa mwisho wa ligi Jumapili hii, siku tatu kabla ya mchezo wao wa fainali ya Europa League. Ushindi dhidi ya Ajax Amsterdam jijini Stockholm Jumatano ijayo, utaifanya United kupata nafasi ya moja kwa moja katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao. Akizungumza na wanahabari, Mourinho amesema katika kila nchi duniani mechi ingechezwa Jumamosi, kwani wataendelea kubakia nafasi ya sita kwa matokeo yeyote watakayopata na Palace wako eneo salama. Mourinho aliendelea kudai kuwa katika kipindi cha miaka saba aliyokaa Uingereza hajabahatika kuona jitihada zozote za kujaribu kuzisaidia timu za hapo zinapokuwa katika mashindano ya Ulaya.

No comments:

Post a Comment