Thursday, June 22, 2017

BALOTELLI KUBAKIA NICE.

RAIS wa Nice, Jean-Pierre Rivere amedai kuwa Mario Balotelli yuko tayari kubakia katika klabu hiyo hata kwa kupunguziwa mshahara wake. Balotelli ambaye alitua Nice Agosti mwaka jana akiwa mchezaji huru kufuatia kuachwa na Liverpool, mkataba wake unatarajiwa kumalizika wiki ijayo. Baada ya kufunga mabao 15 msimu uliopita na kuiwezesha Nice kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligue 1, nyota huyo wa kimataifa wa Italia anataka kuendelea kubakia hapo pamoja na kuwaniwa na Marseille na timu kutoka Uturuki. Akizungumza na wanahabari mapema leo, rais huyo amesema Balotelli ataka kuendelea kubakia Nice na yuko tayari kushiorikiano nao kifedha ili aendelee kufanya nao kazi.

No comments:

Post a Comment