Friday, June 23, 2017

SALAH APEWA NAMBA YA COUTINHO LIVERPOOL.

KLABU ya Liverpool imefanikiwa kukamilisha usajili wa winga wa zamani wa Chelsea Mohamed Salah kutoka AS Roma. Nyota huyo wa kimataifa wa Misri mwenye umri wa miaka 25, amesaini mkataba wa miaka mitano na alikuwa chaguo namba moja la meneja Jurgen Klopp. Kiasi hicho cha usajili kimeshindwa kufikia rekodi ya paundi milioni 35 Liverpool ilizolipa kwa ajili ya Andy Carroll mwaka 2011 lakini kimefikia kiasi alichosajiliwa Sadio Mane mwaka 2016. Mwaka 2014 Salah ilibaki kidogo atue Anfield akitokea FC Basle lakini dili hilo lilishindikana na kwenda Chelsea.

No comments:

Post a Comment