Friday, June 23, 2017

NEYMAR ATENGANA NA MPENZI WAKE.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Neymar ametangaza kutengana na mpenzi wake Bruna Marquezine. Nahodha huyo wa kimataifa wa Brazil alirudiana na mpenzi wake huyo mwigizaji mwaka jana baada ya wawili kutengana mara ya kwanza mwaka 2014, ambapo Marquezine alikuwepo kushuhudia Neymar akiongoza nchi yake kutwaa medali ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki iliyofanyika katika ardhi yao. Hata hivyo, akizungumza na wanahabari jijini Sao Paulo katika shughuli ya hisani, Neymar alikiri kuwa kwa mara nyingine wameamua kutengana. Neymar amesema huwa hapendi kuzungumzia masuala binafsi lakini ni kweli ameachana na Bruna na ilikuwa makubaliano ya pande zote mbili.

No comments:

Post a Comment