Monday, June 26, 2017

BALOTTELLI AONGEZA MKATABA NICE.


MSHAMBULIAJI wa Nice, Mario Balotelli amesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja na klabu hiyo ya Ligue 1. Nyota huyo wa kimataifa wa Italia, mwenye umri wa miaka 26, amefunga mabao 15 katika ligi msimu uliopita na kuiwezesha Nice kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye msimamo na kufuzu hatua ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao. Balotelli alisajiliwa na klabu hiyo akiwa mchezaji huru kutoka Liverpool Agosti mwaka jana, miaka miwili baada ya kusajiliwa Anfield kwa kitita cha paundi milioni 16. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester City pia amefunga mabao 13 katika mechi 33 alizoichezea timu ya taifa ya Italia lakini hajaitwa katika kikosi hicho toka kumalizika kwa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014.

No comments:

Post a Comment