Tuesday, June 20, 2017

DANI ALVES ANUKIA MAN CITY.

BEKI wa kimataifa wa Brazil, Dani Alves anadaiwa kukubali mkataba wa miaka miwili na Manchester City na uhamisho wake unatarajiwa kuthibitishwa pindi mazungumzo ya kuvunja mkataba wake Juventus yatakapokamilika. Alves alikutana na maofisa wa Juventus jana mchana ili kueleza mpango wake wa kuondoka. Taarifa zinadai kuwa City wanaweza kulipa kiasi kidogo cha fedha kinachokadiriwa kufikia paundi milioni tano kwa ajili ya kunasa saini beki huyo. Taarifa kutoka nchini Italia zinadai kuwa Alves atakuwa akilipwa kiasi cha paundi milioni 4.3 kwa mwaka kiasi ambacho bdio ofa aliyopewa Nolito majira ya kiangazi mwaka jana.

No comments:

Post a Comment