Thursday, June 29, 2017

DEFOE AREJEA TENA BOURNEMOUTH.

MSHAMBULIAJI wa Sunderland, Jermain Defoe amesajiliwa tena na klabu yake ya zamani ya Bournemouth akiwa mchezaji huru. Nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 34, ambaye amesaini mkataba wa miaka mitatu amesema amefurahi kurejea tena katika Uwanja wa Vitality. Defoe alifunga mabao mabao 15 katika Ligi Kuu msimu uliopita aliendelea kudai ulikuwa uamuzi rahisi kujiunga na klabu kubwa yenye kocha bora. Defoe anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Bournemouth baada ya ujio wa kipa Asmir Begovic aliyetokea Chelsea. Bournemouth ilimaliza katika nafasi ya tisa katika msimamo katika msimu wao wa pili katika Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment