Thursday, June 29, 2017

VIONGOZI WA TFF, SIMBA WAPANDISHWA KIZIMBANI.

RAIS wa Shirikisho la Soka nchini-TFF Jamal Malinzi na Katibu Mkuu Celestine Mwesigwa wamesomewa mashitaka 28 katika Mahakama ya Kisutu mapema leo. Viongozi hao walikamatwa mapema jana kwa mahojiano na TAKUKURU kabla ya kufikishwa mahakamani mapema leo. Malinzi na Mwesigwa wote wamerudishwa rumande mpaka Jumatatu ijayo ya Julai 03 ambapo dhamana yao ndio itajadiliwa kutokana na makosa yanayowakabili. Wakati huohuo, Rais wa klabu ya Simba Evans Aveva na Makamu wa Rais, Geofrey Nyange “Kaburu” nao wamerudishwa rumande mpaka Julai 13 baada ya kusomewa mashitaka matano ikiwemo utakatishaji fedha. Aveva na Kaburu nao waliitwa na TAKUKURU kwa mahojiano kama ilivyokuwa kwa Malinzi na Mwesigwa.

No comments:

Post a Comment