Thursday, June 22, 2017

JUVENTUS KUMUACHIA DANI ALVES.

KLABU ya Juventus imethibitisha itamuacha beki wake wa kulia Dani Alves pamoja na kuwa amebakisha mkataba wa mwaka mmoja. Meneja huyo wa Manchester City, Pep Guardiola anadaiwa kumuwania nyota huyo mwenye umri wa miaka 34, ambaye walikuwa wote Barcelona. Ofisa mkuu wa Juventus, Beppe Marotta amesema Alves anataka kutafuta changamoto mpya hivyo ana matumaini watafikia muafaka kwenye suala lake ili aweze kutimiza ndoto zake. Marotta aliendelea kudai kuwa wanamtakia kila la heri beki huyo ambaye wamekuwa naye kwa kipindi cha mwaka mmoja.

No comments:

Post a Comment