Tuesday, June 20, 2017

USAJILI WA SALAH WANUKIA LIVERPOOL.

WINGA wa kimataifa wa Misri, Mohamed Salah anategemewa kukamilisha usajili wake kwenda Liverpool akitokea AS Roma Alhamisi baada ya kutua nchini Uingereza leo kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya. Taarifa zilizotoka jana zimedai kuwa Liverpool bado wanamalizia majadiliano na Roma kuhusu uhamisho huo unaotarajiwa kuwagharimu kiasi cha paundi milioni 39. Usajili huo ukikamilika utakuwa umezidi ule wa Andy Carroll wa paundi milioni 35 uliofanyika Januari mwaka 2011. Kama kila kitu kikienda kama kilivyopangwa mpaka ifikapo Juni 22 Salah mwenye umri wa miaka 25 atakuwa amesaini mkataba wa miaka mitano ambao utamfanya kukunja kitita cha paundi 90,000 kwa wiki.

No comments:

Post a Comment